Ujumbe nilioutuma umekwama angani
Kunani?wingu limefunika kazkazini
Kipepeo nilichokipepesa kinjiani
Kuwa na ari nakwambia atakuwezesha Rabuka
Namwomba Rahima aondoe mashaka
Ninasidi nakusakasaka sadaka
Mola hatanitupa langu litafika
Kuwa na ari nakwambia atakuwezesha Rabuka
Miezi na siku nimevumilia
Naamini dua langu utalikubalia
Usiku, mchana furaha kuipalilia
Kuwa na ari nakwambia atakuwezesha Rabuka
Nimeyaamini ya Rahima kweli mapenzi
Kanitunuku ya kweli kipanzi
Kwake nitavumilia japo ni kazi
Kuwa na ari nakwambia atakuwezesha Rabuka
Vumilia Kwa Hasira Na Hasara
Didachus Nyaundi
(C) All Rights Reserved. Poem Submitted on 11/04/2022
(1)
Poem topics: , Print This Poem , Rhyme Scheme
<< Bahati Haivutwi Kwa Kamba Poem
Next Poem
Write your comment about Vumilia Kwa Hasira Na Hasara poem by Didachus Nyaundi
Best Poems of Didachus Nyaundi